• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • MMM
    • Barua pepe za Watumishi
Local Government Loans Board

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Bodi ya Mikopo ya Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Makatibu Waliowahi Kuongoza Bodi
    • Orodha ya Wajumbe wa Bodi
    • Orodha ya Mawaziri TAMISEMI
  • Huduma
    • Huduma Zetu
  • Utawala
    • Muundo
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Kanuni
    • Kuomba Mkopo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Miradi
    • Miradi iliyokwisha
    • Mwongozo wa Uombaji wa Mkopo

LAAC: HATUTAKUBALI SERIKALI IPATE HASARA

Posted on: March 21st, 2024

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) imesema itahakikisha inasimamia ipasavyo matumizi ya fedha za umma zilizopelekwa kutekeleza miradi kwenye maeneo mbalimbali na hawatakubali Serikali ipate hasara.

Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC)  Mhe. Ester Bulaya ameyasema hayo Machi 21, 2024 katika kikao cha majumuisho ya ziara walioifanya Kamati hiyo katika Manispaa ya Moshi, Mkoani Kilimanjaro ya ukaguzi wa jengo la halmashauri, ujenzi wa shule ya sekondari na stendi ya Manispaa ya Moshi.

Ameeleza pamoja na kuonekana kwa  ubora wa ujenzi wa miradi  katika Mkoa wa Kilimanjaro,  Kamati ya  LAAC inajukumu la kufuatilia fedha za Serikali ili zifuate  utaratibu katika matumizi yaliyopangwa  kwa kuzingatia miongozi, taratibu na sheria za Serikali na kutoka Ofisi ya Rais -TAMISEMI.

“Naibu Katibu Mkuu ( Elimu) mtu ambaye amekiuka taratibu  lazima ashughulikiwe nchi hii ni kubwa unapopata fursa ya kusimamia fedha za miradi lazima tusimamie ilete tija kwa wananchi,” amesisitiza Mhe. Bulaya

Akisoma maazimio ya Kamati hiyo, Mjumbe wa LAAC, Mhe. Hawa Mchafu(Mb), amesema Kamati imemtaka Mkurugenzi kuhakikisha kasi ya mradi wa jengo la utawala la Halmashauri hiyo inaongezeka  na kukamilika ndani ya muda wa mkataba   tarehe 28 Machi 2024.

Amesema Kamati imemtaka Mkurugenzi kuhakikisha utekelezaji wa miradi unazingatia sheria, kanuni na taratibu inayotolewa na Serikali ikiwa ni pamoja na kujenga kulingana na michoro illyotolewa na Ofisi ya Rais -TAMISEMI.

Pamoja na maekelezo mengine Kamati pia  imeitaka Ofisi ya Rais -TAMISEMI ichukue hatua kwa watu wote  waliohusika kwa ukiukwaji wa sheria wakati wa kuingia mkataba wa ujenzi wa stendi.

Naye,  Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – TAMISEMI Dkt. Charles Msonde  ameahidi Ofisi ya Rais – TAMISEMI itasimamia kwa karibu  maelekezo yote ya  Kamati iliyoyatoa na yatatekelezwa ikiwamo kuundwa kwa timu ya kufanya tathmini ya ujenzi wa mradi wa stendi ya Manispaa ya Moshi  ili hatua zichukuliwe na wananchi wapate huduma.

Matangazo

  • RAIS SAMIA AIWEZESHA REA BILIONI 96.8 UTEKELEZAJI MIRADI YA UMEME VIJIJINI DODOMA May 13, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU WAHITIMU WA KIDATO CHA NNE,2023 KUFANYA MABADILIKO YA TAHASUSI ZA KIDATO CHA TANO NA KOZI ZA VYUO KWA MWAKA 2024 March 20, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MWENENDO WA UREJESHAJI MIKOPO KWENYE HALMASHAURI UNARIDHISHA - DKT. FESTO DUGANGE.

    May 08, 2025
  • MAFUNZO YA UANDISHI BORA WA MAANDIKO YA MIRADI ILI KUZIWEZESHA MAMLAKA ZA SERIKALI ZA MITAA KUPATA PESA ZA MIRADI YA KIMKAKATI

    March 08, 2024
  • MAANDIKO BORA KUZIWEZESHA MAMLAKA ZA SERIKALI ZA MITAA KUPATIWA MIKOPO KWENYE TAASISI ZA FEDHA

    March 25, 2024
  • LAAC: HATUTAKUBALI SERIKALI IPATE HASARA

    March 21, 2024
  • Angalia Zote

Wasiliana Nasi

Local Government Loans Board

Sanduku la Barua: P.O Box 2710

Simu: +255 26 2321730

Barua Pepe: barua@lglb.go.tz

Fax:

Viungo vya Haraka

  • Watumishi Portal
  • President's Office, Regional Adminstration and Local Government
  • MATUKIO

Zinazohusiana

  • Chuo cha Serikali za Mitaa
  • OR-TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • TAMISEMI BLOG
  • Benki ya Maendeleo (TIB)

Video Mpya

More Videos
    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Sitemap
    • Huduma

Haki Miliki@ Bodi ya Mikoya Mikopo ya Serikali za Mitaa